Loading...

Elimu ya lazima

Programu inayolenga kwa ujumla Waislamu wanaotaka kupokea elimu ya kisheria ya lazima, (yanayojulikana katika dini kwa lazima, nayo ni yale ambayo haimpasi Muislamu kutoyajua), kwa isnadi (Mapokezi) yenye kuungana, ambapo programu hii inajumuisha idadi ya masomo yanayowasilishwa kwa mujibu wa mpangilio wa kielimu uliomzuri na kwa njia rahisi na nyepesi, na masomo yake yako wazi na hayajafungwa kwa muda maalumu, Mwanafunzi anaweza kupitia humo kujisajili na kusoma masomo na kuyakamilisha katika wakati na muda unaomfaa yeye.

Video ya utangulizi wa Program

Jinsi ya kusoma

Idadi ya viwango vya programu: Ni kiwango kimoja tu, kinachojumuisha mitaala mitatu, lazima mwanafunzi aanze na mtaala wa Yanayojulikana katika dini kwa lazima kisha mtaala wa Tauhid na tabia kisha mtaala wa Fiqhi. 

Masomo yako wazi muda wote bila kuhusishwa na muda maalumu. Mwanafunzi anaweza kuyapata masomo wakati wowote na kumaliza wakati wowote kwa mujibu wa nafasi yake.

Mwanafunzi akiingia tu katika ukurasa anaanza moja kwa moja kusoma masomo yote yaliyopo, na anaweza kuyaona masomo wakati wowote autakao. Akimaliza kitabu, akitaka anaweza kufanya mtihani na kuendelea na kitabu kingine.

Mwanafunzi akipata ufaulu uisopungua 70% katika kitabu cha Mtaala, anapewa cheti cha kukamilisha programu.

— Mtihani wa somo: Mtihani unakua kwa njia ya maswali ya kuchagua (Chagua jibu sahihi) baada ya kila somo, na wastani wa ufaulu ni 80%.

— Hakuna mitihani ya mwezi au Katikati ya mwezi, bali kuna mtihani wa mwisho tu kwa kila kitabu, Nayo ni mitihani ya kielektroniki, kwa kuwepo nafasi maalumu kwa ajili ya mitihani hiyo mwisho wa somo kwa kila kitabu, na inamwezekania mwanafunzi akimaliza kusoma kitabu cha mtaala akafanya mtihani wake kwa muda autakao yeye na yatatumwa kwake moja kwa moja Matokeo na uthibitisho