Loading...

Katika mfumo wa mpango wa Chuo cha Sanad wa kueneza elimu na kupanua wigo wa wanufaika duniani kote.. Wanafunzi kutoka katika kozi ya wanaozungumza Kiingereza watembelea chuo na kujadili fursa za ushirikiano

01/09/2026
Matembezi

Chuo cha Sanad cha Elimu ya Sharia, lango la kidijitali la Darul Mustafa ya Masomo ya Kiislamu Tarim, kilipokea idadi ya wanafunzi wanaozungumza Kiingereza, walioshiriki katika kozi ya 32 ya kiangazi katika Darul Mustafa ya Masomo ya Kiislamu Tarim. Hilo lilifanyika katika mfumo wa kukitambulisha Chuo, programu zake, na kutafuta njia za kupanua manufaa yake katika nchi mbalimbali Duniani.

Wakati wa ziara hiyo, wanafunzi walitambulishwa kuhusu Chuo cha Sanad, dira yake na programu zake za kielimu, pamoja na maudhui ya kielimu yenye kuaminika inayotokana na mfumo wa Darul Mustafa ya Tarim, kupitia jukwaa la kidijitali linalowawezesha wanafunzi kunufaika na elimu ya Sharia popote walipo.

Aidha, katika mkutano huo zilijadiliwa fursa za ushirikiano wa pamoja, na kuwekwa mawazo yatakayochangia kukitambulisha Chuo na kueneza programu zake miongoni mwa Waislamu wa nchi za Magharibi. Hilo litachangia kufikisha elimu ya Sharia yenye kuaminika kwa kundi kubwa zaidi la wanafunzi na wenye shauku ya elimu, sambamba na wanafunzi walioshiriki kunufaika na programu za Chuo na kuendelea na safari yao ya kielimu kupitia jukwaa lake.

Hatua hii imekuja katika mwelekeo wa Chuo cha Sanad wa kupanua uwepo wake Duniani kote, na kujenga madaraja ya ushirikiano na wanafunzi wa elimu, taasisi na vituo vya Kiislamu katika nchi mbalimbali Duniani.

Chuo cha Sanad kinatoa programu zake za kielimu kwa lugha tatu: Kiarabu, Kiingereza na Kiswahili, jambo linalokiwezesha kuyafikia makundi mbalimbali ya wanafunzi wa elimu duniani kote. Njia ya Kiingereza inajumuisha kundi la walimu mahiri wa Chuo kutoka Amerika, Ulaya, Australia na Afrika Kusini. Kadhalika, katika Lugha ya Kiswahili wapo walimu kutoka Afrika Mashariki, Kenya na Tanzania, katika mwendelezo unaoakisi mwelekeo wa Chuo wa kutoa elimu ya Sharia yenye kuaminika kwa wanafunzi katika mazingira yao na kwa lugha zao mbalimbali.